Baada ya kutoonekana kufanya kazi na CEO wa WCB, Diamond Platnumz hatimae aliyekua videographer na mpiga picha rasmi wa msanii huyo, Lukamba ameweka wazi kuwa hafanyi tena kazi na bosi wake huyo.
Lukamba ambaye kwa sasa amegeukia muziki amefunguka hayo akiongea na waandishi wa habari na ameeleza kuwa ameacha rasmi kufanya kazi na Diamond.
Lukamba amesema kuwa kwa sasa amefungua kampuni yake mpya huku akiongeza kuwa kufanya kazi tena na msanii wa Tanzania itakua ngumu labda awe mkubwa kumzidi Diamond, huku akiwataja wasanii kama Davido na Wizkid kama watahitaji kufanya nae kazi basi hatokataa.