Menu ›
Burudani
Fri, 11 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mapema leo, Rapa Tekashi 6ix9ine alikamatwa huko Palm Beach, Florida nchini Marekani.
Mamlaka za usalama zinaeleza kwamba, Kuna dereva alisimamishwa barabarani na baadaye kutambulika kuwa ni Daniel Hernandez (6ix9ine) ambaye leseni yake ilisimamishwa.
Tekashi pia alikutwa na ‘mkeka’ wa makosa ya barabarani ambao aliwahi kuandikiwa kwa kushindwa kufika Mahakamani kwa kosa la kukutwa na gari ambalo halijasajiliwa.
Aidha taarifa zinaeleza kwamba, rapa huyo mwenye majivuno ameachiwa kwa dhamana ya ($2,000) takribani Tsh. Milioni 5.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live