Menu ›
Burudani
Fri, 22 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rapa Quavo amekutana na Makamu wa Rais wa Marekani, Bi. Kamala Harris kwenye Ikulu ya White House na kuzungumza naye masuala kadhaa ikiwemo la kudhibiti vurugu na uhalifu wa silaha nchini humo.
Quavo amemwambia Kamala kwamba hataki mtu wake mwingine wa karibu auawe kwa risasi kama ndugu yake TakeOff ambaye aliuawa Novemba 1, 2022.
“Sitaki hii itokee kwa mtu mwingine. Ninataka kupunguza chini kabisa hizi asilimia. Tunapaswa kufanya vizuri kwenye kudhibiti silaha.” alisema Quavo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live