Staa wa filamu Bongo, Rammy Galis ametaja sababu ya kuachana na aliyewahi kuwa mpenzi wake kipindi cha nyuma, Poshy Queen.
"Ni kweli nilikuwa kwenye mahusiano na Poshy Queen lakini niliachana nae baada ya kukosa kile nilichokitarajia. Nimejifunza mwanamke kuwa na makalio makubwa.
"Urembo wa sura sio kipimo cha akili nyingi ya maisha, na kwa nyakati hizi wanaume tunahitaji mwanamke mwenye akili ya kutafuta hata baba ukipata shida mama aweze kupambania watoto akupambanie na wewe mwenyewe.
"Lakini ukioa mwanamke mwenye makalio makubwa alafu hana akili utaumia, hivyo niliachana nae na nipo kwenye mahusiano na mtoto wa Kinyarwanda, msomi na mwelevu, na ninafanya kazi kwenye kampuni ya baba yake (Mkwe wangu) kampuni inayojihusisha na mambo ya kuendesha ndege," amesema Rammy Galis.