Msanii wa muziki, Linah Sanga amefunguka kwa kusema kuwa alikaa chini na mwanadada Rachel Kizunguzungu na kumueleza nini anatakiwa kufanya ili asiyumbe kama mwaka 2017.
Linah akiwa na rafiki yake Rachel
Muimbaji huyo ambaye ni mama wa mtoto mmoja kwa sasa, amedai baada ya kumuona rafiki yake Rachel amepotea kwenye muziki kwa muda mrefu, alimua kumtafuta mrembo huyo na kukaa naye chini katika hatua nzuri ya kumueka sawa.
“Rachel ni rafiki yangu mkubwa, toka tukiwa THT tulikuwa pamoja na tulifanya kazi kwa kushirikiana sema hivi karibuni mwenzangu amekutwa na misukosuko ya maisha kitu ambacho ni cha kawaida katika maisha ya binadamu,” Linah aliimbia Bongo5.
“Lakini tayari nimeshakaa naye na tumezungumza mambo mengi na tumeelewana mwaka 2018 kwa Rachel utakuwa wa tofauti kabisa,” aliongeza.
Wawili hao tayari wameshaingia studio kwaajili ya kuandaa wimbo wao wa pamoja.