Menu ›
Burudani
Sat, 20 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz ameshangazwa na uwezo wa mtoto mwenye ulemavu wa macho huko nchini Rwanda baada ya mtoto huyo kuimba nyimbo zake mbili ile hali hata hajui lugha ya kiswahili.
Diamond Platnumz ambaye yupo nchini Rwanda kwa ziara yake binafsi ameshangazwa na mtoto huyo kwenye kituo cha kulelea watoto wenye ulemavu wa macho (Vipofu) cha Jordan Foundation huko Gatsata, Jijini Kigali.
Tazama mtoto huyo alivyomkosha Diamond Platnumz kwa kuimba nyimbo mbili za Je, Utanipenda na Marry You. (Video by Igihe Tv)
Chanzo: bongo5.com