Mwimbaji Nyota wa R&B kutoka Chicago, ameondolewa mashtaka ya Jinai kuhusu Unyanyasaji wa Kijinsia yaliyotakiwa kusikilizwa Mahakamani leo Januari 31, 2023.
Uamuzi huo umetokana na kifungo cha Miaka 30 ambacho R Kelly anatumikia baada ya kupatikana na hatia katika kesi nyingine za Ulanguzi wa Kingono huku akikabiliwa na kifungo cha ziada kupitia kesi ya kuhifadhi Ponografia za Watoto.
Septemba 2022, Mahakama ya Chicago lilimtia hatiani Kelly kwa makosa 6 ya Ponografia na Kushawishi Watoto wadogo kushiriki katika shughuli za uhalifu wa Kingono ambapo hukumu yake imepangwa Februari 23, 2023