Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Quick Rocka akabidhiwa mshindi wa BSS 2019, Ritha aomba radhi

BSS Quick Rocka akabidhiwa mshindi wa BSS 2019, Ritha aomba radhi

Mon, 17 Aug 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Msanii wa Bongo Fleva, Quick Rocka ametangazwa rasmi kuwa meneja mshindi wa shindano la Bongo Star Search (BSS) 2019, Meshack Fukuta.

Hilo limeelezwa jana Jumapili Agosti 16, 2020 na Mkurugenzi wa BSS, Ritha Paulsen katika uzinduzi wa shindano hilo msimu wa 11 uliofanyika Jijini Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine, Mkurugenzi wa mashindano hayo, Ritha Paulsen, amesema tayari wamemalizana na msanii huyo kuhusu zawadi pamoja na kumtafutia menejimenti ya kumsimamia kazi zake kama walivyoahidi.

Akizungumzia kuhusu hatua hiyo, Meshack amesema amefurahi kumpata meneja ambaye ni mtu sahihi katika soko la muziki kwa sasa.

"Unaweza kuwa msanii mzuri,lakini mwisho wa siku ukatunga nyimbo zako na kuzirekodi ukabaki nazo ndani kama huna mtu wa kukushika mkono.

"Kwangu kaka yangu Quick Rocka ni mtu sahihi,nina imani kwa ushirikiano wetu nitaweza kufika ndoto zangu za kuwa msanii mkubwa na hatimaye kuibua wengine kama nilivyoinuliwa mimi,"amesema.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz