Msanii wa muziki Bongo na Mbunifu wa mavazi, Q Boy Msafi amefunguka kuhusu ukaribu wake na Young Dee kwa sasa pamoja na kubadili mfumo wake wa kazi tangu alipoondoka WCB.
Muimbaji huyo ameiambia Bongo5 kuwa kwa sasa haonekana na Young Dee baada ya kumalizika mkataba wao na pia anafanya biashara zake binafsi.
“Tupo vizuri tunachekiana tu, sema moja ya vitu ambavyo nina focus navyo nimefungua duka langu, pia kuhakikisha ni kwa namna gani wateja wangu wanaweza kupendeza na kuwa na muonekano mzuri,” amesema.
“So nakuwa upande wangu wa pili tofauti na zamani nilikuwa na mkataba na menejimenti yake ila sasa mkataba umeisha,” ameongeza Q Boy Msafi.