Msanii wa muziki wa hip hop kutoka King Cash, Young Dee amefunguka kwa kusema kuwa profile yake katika muziki wa BongoFleva ndiyo kitu pekee ambacho kinaweza kumpeleka kimataifa.
Young Dee
Rapa huyo amesema mwaka 2018 ananza kwa kutengeneza mazingira ambayo yatamfanya awe tofauti na wasanii wote wa muziki Tanzania.
“Msanii ni profile, umefanya nini kwenye muziki?, una umri gani kwenye muziki na ume-share jukwaa moja na wasanii gani wakongwe na wakubwa duniani, una albamu ngani. Binafsi sitaki kujikweza sana lakini huu mwaka nataka kufanya vitu vikubwa sana, kwa sababu profile yangu inaniruhusu kufanya hivyo” alisema Dee.