Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Professa Jay awaonya wanaoimba matusi

C6b6634ae5a709ebb6bbfd1ae4539ff4.jpeg Professa Jay awaonya wanaoimba matusi

Sat, 12 Jun 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya Joseph Haule ‘Profesa Jay’ amewaonya wasanii wanaoimba matusi kubadilika na kuwahimiza kuzingatia maadili.

Akizungumza na gazeti hili Dar es Salaam juzi Profesa Jay alisema vijana wengi wanaochipukia wanaimba muziki ambao mtu akikaa na familia kuangalia ni aibu tupu.

“Hawa watoto wanaochipukia wamebadilisha muziki, wengi wanaimba matusi na mara nyingi nimekuwa nikikemea kwa sababu kuna vitu vingine ni aibu huwezi kuangalia na familia,” alisema.

Alisema sababu ya kukemea mara kwa mara wanaoimba matusi ni kujaribu kuwakumbusha kuzingatia maadili.

Katika hatua nyingine, msanii huyo alisema wiki ijayo anatarajia kuachia kibao kipya kuonesha mashabiki kuwa bado yupo.

Alisema ataendelea kutoa wimbo mmoja kila baada ya muda ili ifikapo mwishoni mwa mwaka huu awe na hazina kubwa ya nyimbo kwa ajili ya albam.

Professa Jay alisema albamu hiyo itakuwa na nyimbo atakazoshirikiana na wasanii kadhaa wa nyumbani na wengine wa nje ya nchi na hivi karibuni ataanza safari za kimataifa.

Chanzo: www.habarileo.co.tz