MSANII wa Bongo Fleva, Joseph Haule, ‘Profesa Jay’, amesema ana mipango wa kuachia kazi ili kuendelea kuwafurahisha mashabiki wake.
Profesa Jay alitoa kauli hiyo siku chache baada ya kushirikishwa kwenye wimbo wa ‘Baba‘ unaovuma akishirikishwa na msanii Boniventure Kabongo ‘Stamina’.
Kupitia kwenye mtandao wake wa Instagram, Profesa Jay aliwajulisha mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwani mipango yake kwa sasa nikuachia kazi .
“Nadhani sasa umewadia muda muafaka wa kuachia nyimbo mpya, kuachia kazi baada ya kazi ili kuwafurahisha mashabiki wangu kama ilivyokuwa miaka ya nyuma,” alisema Profesa Jay
Profesa Jay ambaye alikuwa mbunge wa Mikumi alisema shughuli za kuwawakilisha wananchi zilikuwa zinamkosesha muda wa kutunga nyimbo hivyo anaamini kwa sasa ana muda wa kutosha kuendelea na tasnia hiyo.