Menu ›
Burudani
Mon, 20 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Binti wa kwanza wa Malkia Rania na Mfalme Abdullah II wa Jordan, Princess Iman alifunga pingu za maisha na Jameel Thermiotis tarehe 12 mwezi huu katika Mji Mkuu wa Jordan, Amman.
Thermiotis ni mzaliwa wa Venezuela ambaye mababu zake wana asili ya Kigiriki.
Ili kumuoa binti Mfalme Mfanyabiashara huyo mwenye makazi yake Jijini New York nchini Marekani, alilazimika kubadili dini na kuwa Muislamu, hivyo kubadili jina lake na kuwa Jameel.
Harusi yao ilikuwa ya Kifahari zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Jordan. Baada ya harusi hiyo wawili hao wameenda kuanza maisha yao jijini New York.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live