Menu ›
Burudani
Sat, 28 Apr 2018
Chanzo: bongo5.com
Rick Ross tayari ametua ndani ya Kenya kwa ajili ya kufanya show yake ya kufa mtu April 28 ya mwaka huu.
Bosi huyo wa Maybach Music Group, amepokelewa kwa shangwe kubwa kwenye uwanja wa ndege wa nchini humo ikiwa ni mara yake ya pili kutia Afrika Mashariki baada ya kutua Bongo kwenye tamasha la Fiesta jijini Dar es Salaam Oktoba mwaka 2012.
Rick Ross anatarajiwa kupanda jukwaani na wasanii wengine wa Kenya akiwemo Khaligraph Jones na Nyashinski kutoka Kenya.
Chanzo: bongo5.com