Baada ya tetesi za muda mrefu kuwa Kylie Jenner, ni mjamzito na huwenda ndiyo mbeba mimba wa Kim Kardashian hatimaye mrembo huyo wa Travis Scott ameonekana kwa mara ya kwanza katika picha ya pamoja na ndugu zake huku akiwa na mavazi ya Calvin Klein.
Wiki kadhaa zilizopita tuliona Khloe Kardashian, Kendall, Kourtney na Kim wakiziachia picha mbalimbali wakiwa na watoto wao katika mavazi ya Calvin Klein katika mitandao ya kijamii, lakini Kylie hakufanya hivyo hata kidogo tokea alipotangaza mwaka jana kuwa na ujauzito.
Picha hizo zimemuonyesha Kylie akiwa amevaalia mavazi ambayo ni makubwa tofauti na wenzake. Hali inayoendela kuleta sinto fahamu kwa mashabiki zake.