Menu ›
Burudani
Fri, 1 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwimbaji Peter Msechu ametoa wimbo maalum wa kumuaga Rais mstaafu Hayati Mzee Ali Hassan Mwinyi uitwao ‘lala salama Ali Hassan Mwinyi’
Katika wimbo huo Msechu ameanza kwa kuutanguliza usemi maarufu wa Mzee Mwinyi aliowahi kunukuliwa akisema “maisha ya Mwanadamu ni hadithi tuu hapa ulimwenguni, basi eee Ndugu yangu kuwa hadithi nzuriii”
Hayati Ali Hassan Mwinyi amefariki jana Hospitalini Jijini Dar es salaam baada ya kuugua kansa ya mapafu ambapo amefariki miezi miwili kabla ya kumbukizi ya siku yake ya kuzaliwa ( May 8) ambapo angefikisha umri wa miaka 99.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live