Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Penzi la Wema Sepetu lachanua upya, Diamond atajwa

5021 Wpid Wema Akiwa Pembeni Kumsupport Diamond1 E1521208044654 TZW

Tue, 20 Mar 2018 Chanzo: bongo5.com

Mapenzi ni kikohozi, hayawezi kufichika. Malkia wa filamu nchini Tanzania Wema Sepetu Jumatatu hii amepost picha ya ua la rose “Red Rose’ ambalo linadaiwa kuwa ni ishara ya upendo.



Mwigizaji huyo amekaa kimya kwa muda mrefu bila kuweka wazi mahusiano yake toka aachane na mchekeshaji Idris Sultan kitu ambacho siyo kawaida yake katika maisha yake.

Jumatatu hii amepost ua jekundu ikiwa ni ishara ya upendo huku akiandika ujumbe unaosomeka ‘A Red Rose is a Symbol of Love…’.

Hatua hiyo imechukuliwa tofauti na mashabiki wengi wa mrembo huyo baada ya hivi karibuni kuonekana kuwa karibu zaidi na mpenzi wake wa zamani, Diamond Platnumz.

Mashabiki hao wengi kupitia Instagram muda mchache baada ya mrembo kupost ua, amekuwa wakimtania kwa kusema kwamba huwenda mrembo huyo ameamua kurudia na Diamond ambaye ameachana na mama watoto wake, Zari The Boss Lady.

Maoni na mashabiki hao kupitia instagram.

udankimario

Madame wema nahisi kwa upande wa pili itakua ni Special kwa A boy From Tandale yan Simba

Chanzo: bongo5.com