Kulikuwa na uvumi kwamba huwenda Paula asiwe na furaha sana kwa kitendo cha mama yake Kajala Masanja kurudiana na mpenzi wake Rajabu Abdul 'Harmonize' sasa habari ikufikie tu, binti wa watu hana kinyongo chochote na amempongeza mama yake kwa hatua aliyoipiga. Mpango mzima umefanyika usiku wa kuamkia leo kwenye shoo baab'kubwa iliyokwenda kwa jina la Late Luch ambapo Harmonize aliitumia fursa hiyo kumvisha pete asali wa moyo wake, muigizaji Kajala. Ulipofika wakati wa kumpongeza, bila hiyana Paula aliinuka kwa furaha na bashasha tele akaenda kumpongeza na kucha na mama yake kipenzi. Paula ilisadikika hajafurahishwa na kitendo cha mama yake kurudiana na Harmonize kutokana na kosa alilokuwa amelifanya la kumtongoza yeye lakini inaonekana hayo yamepita na sasa wanaganga yajayo.
Kulikuwa na uvumi kwamba huwenda Paula asiwe na furaha sana kwa kitendo cha mama yake Kajala Masanja kurudiana na mpenzi wake Rajabu Abdul 'Harmonize' sasa habari ikufikie tu, binti wa watu hana kinyongo chochote na amempongeza mama yake kwa hatua aliyoipiga. Mpango mzima umefanyika usiku wa kuamkia leo kwenye shoo baab'kubwa iliyokwenda kwa jina la Late Luch ambapo Harmonize aliitumia fursa hiyo kumvisha pete asali wa moyo wake, muigizaji Kajala. Ulipofika wakati wa kumpongeza, bila hiyana Paula aliinuka kwa furaha na bashasha tele akaenda kumpongeza na kucha na mama yake kipenzi. Paula ilisadikika hajafurahishwa na kitendo cha mama yake kurudiana na Harmonize kutokana na kosa alilokuwa amelifanya la kumtongoza yeye lakini inaonekana hayo yamepita na sasa wanaganga yajayo.