Menu ›
Burudani
Thu, 4 Aug 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Sosholaiti na mtoto wa muigizaji Kajala Masanja, Paula ameweka wazi kuwa anaye mpenzi na hataki kuzungumza kuhusu Rayvanny.
Paula amefunguka hayo Agosti 3, 2022 alipokuwa akifanya mahojiano na Wasafi FM kuhusu jambo lake alilopanga kulitangaza siku ya Ijumaa Agosti 5, 2022.
Alisema, anaye mpenzi na asingependa kuulizwa kuhusu Rayvanny ambaye taarifa zinaeleza kuwa walishaachana na sasa kila mtu ana maisha yake.
“Nina boyfriend, nisingependa kumuongelea Rayvanny.”
Hata hivyo, Paula hakuweka wazi kama huyo mpenzi aliyenaye kama ndiye Rayvanny au ni mwingine tofauti.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live