Mwanamuziki kutoka Nigeria Patrick Nnaemeka 'Patoranking' amefichua kuwa ukimya wake kwenye muziki ulitokana na yeye kuwa masomoni.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Patoranking ame-share picha zikifichua kuwa siku chache zilizopita alitunukiwa Shahada 'Degree' kutoka katika Chuo Kikuu cha #Harvard nchini Marekani akiwa ni mmoja wa wanafunzi waliohitimu darasa la BEMS 2024.
Patoranking alieleza kuwa yeye na wengine 35 wamepata Degree in Business, Entertainment, Media, and Sports (#BEMS)’.
Mara ya mwisho #Patoranking kuachia ngoma ni miezi saba aliyopita, aliachia video ya wimbo wake wa ‘Babylon’aliomshirikisha #Victony ukiwa na zaidi ya watazamaji milioni 24.