Baada ya kutoa taarifa katika ziara yake ya #Renaissance kuhusiana na uzinduzi wa #Perfume yake, hatimaye mfanyabiashara na mwanamuziki #Beyonce amezindua manukato hayo ambayo yanapatikana kwa kutoa ‘oda’.
Kupitia ukurasa wa #Instagram wa #Beyonce ame-share promo ya perfume hiyo huku akieleza kuwa manukato hayo yataanza kuingia sokoni Novemba kwa oda.
Manukato hayo yaliyopewa jina la #CENOIR yanapatikana kwa ‘oda’ kwenye tovuti ya mwanamuziki huyo huku bei ya uturi huo ikiwa ni $160 ambapo ni sawa na zaidi ya laki nne za Kitanzania ambapo inadaiwa kuwa manukato hayo yatauzwa Marekani na Canada pekee.
Miezi kadhaa iliyopita #Beyonce na binti yake #BlueIvy walishika vichwa vya habari baada ya kuupiga mwingi katika ziara yao waliyoipa jina la ‘Renaissance World Tour’ iliyoanza May na kutamatika Oktoba 1 mwaka huu.