Lile Shindano maarufu na linalosifika kwa kuibua vipaji nchini Bongo Star Search maarufu kama BSS limerudi tena kwa mwaka 2021.
Usiku wa Septemba 8, 2021 umefanyika uzinduzi wake kwa msimu wa 12 ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Jokate Mwegelo ambaye alipata nafasi ya kufungua zawadi ambayo ilikuwa suprise katika hafla hiyo.
Uzinduzi huo umehudhuriwa na wadau mbali mbali wa masuala ya sanaa na muziki wakimwemo watangazaji na watayarishaji wa muziki.
Lakini katika tukio ambalo limewashangaza wengi ni baada ya kumuona mwanadada mtata Salama Jabir akirudi tena kama Jaji katika mashindano hayo baada ya kutoonekana kwa misimu miwili.