Godfather wa Bongo Fleva P Funk Majani ameonesha kukerwa na tabia za legend wa Bongo Fleva, Q Chief, aandika haya siku chache tangu utoke wimbo mpya 'Malume' aliomshirikisha msanii wa Bongo Records, Rapcha pamoja na Rapa Chidi Beenz.
"Q Chief wewe ni vocalist mkali na performer wa kiwang cha juu kabisa. You are one of the best. Lakini unaniangusha kwa tabia na vitendo vyako. Kuna list ndefu ya wadau waliowahi kukushika mkono na kukupa support kila mtu kwa nafasi yake, kwa namna moja au nyingine mwisho wa siku uliwaangusha."
P Funk ameongeza kuwa, "Inanisikitisha sana kuona kipaji kikubwa hivi kinapotea, nguvu ya kukusaidia na kukufanya uzidi kwende mbele ipo ndani yako pekee."