Baada ya ‘rapa’ P Diddy kutangaza katika Tuzo za BET za 2022 kuwa atatoa dola milioni 1katika Chuo Kikuu cha Howard, hatimaye ametimiza ahadi hiyo ambapo alikabidhi ‘cheki’ ya pesa kwa rais wa chuo Dk. Ben Vinson III.
P Diddy alitoa pesa hiyo wakati wa tamasha chuoni hapo huku katika hotuba aliyoitoa akiwataka wanafunzi kushikamana na kudumisha urithi wa watu wenye ngozi nyeusi.
Licha ya kutoa msaada huo #Diddy aliwaburudisha wanafunzi wa chuo hicho cha watu weusi kwa kutumbuiza baadhi ya ngoma zake ikiwemo ‘I need a girl’.
P Diddy ameonekana katika filamu mbali mbali ikiwemo ‘A raisin in the sun’, ‘Get him to the greek’nk.