Menu ›
Burudani
Fri, 3 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchekeshaji maarufu kutoka Nchini Kenya, Eric Omondi amewasili Nchini Tanzania leo May 02,2024 kwa lengo la kuja kumuunga mkono Msanii Gigy Money ambaye anatarajia kuzindua reality show yake usiku wa leo.
Omond amesema; “Hapa Afrika Mashariki kama kuna Mtu brand ambaye nimemuomba kwa miaka karibu mitano afanye reality show ni Gigy kwasababu she has what it takes, she is the Kim Kadarshian.”
Gigy Money The Reality ni show ambayo inahusu maisha halisi ya Gigy kwa ujumla na itakuwa ikioneshwa kupitia Zamaradi TV kuanzia jana Mei 2, 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live