Msanii wa Bongo Fleva, Omary Nyembo maarufu kama 'Ommy Dimpoz' amekiri fununu kwamba miezi michache iliyopita alifunga ndoa ya kimyakimya na mwanamke wake wa kizungu raia wa Marekani ambaye walikuwa wapenzi kwa muda kabla ya kuwa rasmi kama wanandoa
Dimpoz amebainisha hayo wakati akifanyiwa mahojiano maalum na kituo cha televisheni cha Wasafi TV jana kupitia kipindi cha The Switch.
"Nilifunga ndoa ya kimyakimya na mke wangu ambaye ni raia wa Marekani na tulikutana hukohuko Marekani," amesema Ommy Dimpoz.
Dimpoz amesema kazi yake ya ubunifu(creativity) katika kampuni ya GSM anaifurahia zaidi kuliko hata kazi zake za muziki huku akimshukuru bosi wa GSM kwa kumpa fursa aoneshe uwezo wake.