Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ommy Dimpoz adai kuna wasanii wanatoa nyimbo mbaya, ‘Unaona huu wimbo gani’

7715 26866717 165102110784660 8087184098495299584 N Ommy Dimpoz

Thu, 10 May 2018 Chanzo: bongo5.com

Wasanii wa muziki Bongo, Ommy Dimpoz amesema kuna baadhi ya wasanii ‘wanatoa’ nyimbo mbaya ila wasanii wanzao wanaogopa kuwaambia.



Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na ngoma yake mpya ‘Yanje’ hilo linatokana wale wanaosema ukweli kuchukiwa siku zote.

“Kuna nyimbo za wasanii wenzangu na nyingine unaona huu wimbo gani na unaona mwana anakomaa na ma-intervie,” amesema.

Amesema ni vigumu kumwambia ukweli msanii mwenzako kwamba wimbo wako si kiwango hicho kutokana tayari ameshawekeza.

“Na siku zote wasema ukweli wanachukiwa, kuna siku niko na washikaji jamaa anamwambia mwana lakini ule wimbo wenu mnaenda ku-shoot video?, mbona ngoma mbaya, nikasema unatoa wapi ujasiri wa kumwambia mtu hivyo,” Dimpoz ameiambia Magic FM.

Utakumbuka kipindi cha nyuma Barakah The Prince aliingia kwenye headlines mara baada ya kudai wimbo wa Ben Pol ‘Tatu’ ni mbaya, hata Godzill aliwahi kufanya kitu kama hicho kwa Nay wa Mitego.

Loading...
Chanzo: bongo5.com