Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ombi la Ray C kwa Rais Dkt. Magufuli, ni kuhusu wanawake kuolewa

972 23421382 184230278795009 8659180653201326080 N TZW

Tue, 2 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa muziki Bongo, Ray C ametoa ombi kwa Rais Dkt. John Magufuli kuhusu wanawake kuolewa.

Muimbaji huyo amependekeza kuwa kusiwepo na mahusiano kati ya mwanamke na mwanaume hadi ndoa ili wanawake wengi waweze kuolewa. Kupitia Instagram yake ameandika;

Mzee mi na shida Moja! hawa wanaume hapa nchini wanajifanya wajuaji Sana! Ombi langu la mwaka huu kwako ni hili!Naomba upitishe sheria kama ya Sultan Qaboos wa Oman! Hakuna mahusiano ya Kimapenzi kati ya mwanamke na mwanaume mpaka wafunge ndoa!

Na yeyote atakaekutwa na mwanamke iwe hotelini! Guest house bila Cheti cha ndoa wapelekwe wote segerea!Nadhani itasaidia sana wanawake wengi kuolewa badala ya kuwa manungaembe! Utakuwa umewanyoosha kisawasawa hawa Wanaume zetu Tutaheshimiana!

#NilivyoamkaLeo

July mwaka jana Ray C alikaririwa na kipindi cha FNL cha EATV akisema hayupo katika mahusiano na mtu yeyote kwani ameshapoteza muda katika mambo hayo hivyo hawezi kumpatia mtu nafasi hiyo tena kwani akili yake kwa sasa ameielekeza kwenye kazi.

Chanzo: bongo5.com