Menu ›
Burudani
Thu, 18 Jan 2018
Chanzo: bongo5.com
Kundi la muziki wa Bongo Flava, OMG limefunguka kufanya kolabo na msanii mkubwa kutoka nchini Marekani.
Member wa kundi hilo Con Boi ameiambia Ladha 3600 ya E Fm kuwa bado ni mapema kuweka wazi jina la msanii huyo ila ni kitu ambacho kimeshafanyika.
“Tumefanya kolabo nyingi sana nje ya nchi, watu wa duniani kabisa huko, tumefanya nao. Mapema sana itakuwa sio surprise tena, inabidi kazi zikitoka kuwe na uzito ili kutengeneza ule uzito inabidi vitu viwe vya kushtukiza,” amesema.
OMG kwa sasa wanafanya vizuri na ngoma ‘Wanangu Na Wanao’ ambayo wamemshirikisha Rosa Ree.
Chanzo: bongo5.com