MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Nuh Mziwanda, ameendelea kuomba kutaka kurudiana na aliyekuwa mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ambaye sasa ni mke wa Rommy 3D.
Nuh ambaye hivi karibuni alitoa wimbo wake mpya wa Saudia amesema wimbo huo ni kwaajili ya aliyewahi kuwa mpenzi wake Shilole, huku akisema watu wasimuingilie sababu shida na raha ya mapenzi anayajua yeye.
Alisema anajua kwa sasa yupo na mtu, lakini anaamini hao wote wanapita kwakuwa yeye ni mtu ambaye alichora tatuu yake na kwa sasa yupo tayari kuvumilia kila kitu, ambacho ataambiwa na msanii huyo.
“Eti ooh Shishi mke wangu, sasa akupeleke Ulaya na achore Tattoo kidogo, Saudia Wangu rudi wanakudanganya