Menu ›
Burudani
Wed, 12 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanamitindo maarufu Bongo Noel Ndale, amefunguka kwamba, kuna watu wamezusha kwamba haonekani mara kwa mara na wasanii kama zamani hivyo kuwajibu kwamba yeye sio chawa wa msanii.
Noel amesema, yeye kazi yake ni ubunifu wa mavazi na sio kitu kingine sasa baadhi ya watu huwa wanatamani kwamba kila wakati wamuone ameambatana na wasanii.
“Wabongo wanapenda hayo mambo ya uchawa. Mimi sio chawa. Huwezi kuniona na msanii lakini nipo, naendelea kufanya kazi na wasanii pale ninapokuwepo. Nafanya kazi na Diamond, kama kuna kazi amefanya na sijashariki basi ujue nilikuwa sipo,” alisema Noel.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live