Lifestyle

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

SIL

Nini cha kufanya ikiwa utakutana na chui?

Chui Chui Nini cha kufanya ikiwa utakutana na chui?

Wed, 6 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ripoti za chui kuingia katika makazi ya watu na kuwashambulia huripotiwa mara kwa mara nchini India. Kumetokea mashambulizi mawili ya chui kwenye barabara ya Tirumala hivi karibuni. Mtoto mmoja alipoteza maisha.

Kipi cha kufanya na kipi usifanye ikiwa utakutana na chui? Haya ni maswali yanayoulizwa mara kwa mara.

Siripurapu Madhava Rao, Afisa wa Huduma ya Misitu katika Jimbo la Telangana, anatoa mapendekezo kwa maswali haya.

"Chui kwa kawaida ni paka mwenye haya, hapendi kuonekana na watu. Huondoka anaposikia sauti za watu. Chui anapenda kuishi peke yake. Huonekana tu katika makundi wakati wa kujamiiana,'' alisema.

Chui aina kwa aina

India ina idadi kubwa zaidi ya chuimilia ulimwenguni. Kulingana na takwimu za karibuni zilizotolewa na serikali, idadi yao ni 3682 kufikia 2022. Kwa upande mwingine, idadi ya duma nchini India ni zaidi ya idadi ya chuimilia.

‘’Idadi ya chui wa kawaida huenda ikawa ni karibu elfu 25," anasema. Uharibifu wa makazi, uwindaji na ukosefu wa maji husababisha migogoro kati ya binadamu na wanyama, kwani duma huingia kwenye makazi ya watu, hakuna mnyama anayetoka msituni kwa makusudi, hii inatokana na kuongezeka kwa ushiriki wa binadamu katika msitu.

‘’Kama chui ni mnyama anayetembea kwa kasi, huzua usumbufu mkubwa endapo ataingia katika maeneo yenye watu wengi. Si rahisi hivyo kumkamata chui ambaye ameingia kwenye umati,” anaeleza.

"Njia ya Tirumala kwa kweli ni makazi ya wanyama pori. Kuna wanyama pori wanaohama pande zote za njia. Wanyama wa porini hawawezi kuondolewa huko. Inabidi tuchukue tahadhari. Kitu kama uzio kinapaswa kuwekwa. Au korido zinapaswa kuanzishwa ili kuruhusu harakati za wanyama kutoka pande zote mbili. Vinginevyo makazi yao yataharibiwa," Madhava Rao alisema.

Kipi cha kufanya na kipi usifanye ukikutana na chui?

Hatari hutegemea jinsi chui alivyokaa. Ikiwa amekupa kisogo, huwa hageuki na huendelea na safari yake. Na hana muda wa kushambulia. Uwezekano wa kushambuliwa ni mkubwa ikiwa mnakutana ana kwa ana kwa ukaribu na katika hali ya ghafla.

"Katika hali kama hiyo inua mikono yote miwili na upige kelele kwa nguvu. Anaweza kudhani kuwa wewe ni mnyama mrefu kuliko yeye. Ukiangalia saikolojia ya wanyama pori, kwa kawaida hawashambulii wanyama wakubwa kuliko wao. Katika kesi ya chui, kwa hali yoyote usijaribu kurudi nyuma au kujificha nyuma ya vichaka. Ukifanya hivyo uwezekano wa kushambuliwa ni mkubwa," anasema.

"Haiwezi kusemwa kwa uhakika kwamba atashambulia iwapo utakimbia. Hata hivyo, ikitokea akishambulia, hata ukikimbia kwa kasi kiasi gani, huwezi kushinda mbele ya kasi yake," alieleza.

“Usikimbie ukikutana na duma, kama duma yuko mbali, simama tuli, inua mikono yako, mtazame kisha urudi nyuma taratibu. Ukiinua mikono yako na kupiga kelele na kurudi nyuma polepole kuna uwezekano kwamba duma atarudi nyuma,” aliongeza.

Je, kupanda mti kutakuokoa?

Kupanda miti ni moja ya sifa za kipekee za chui. Anaweza kupanda miti kwa urahisi na kushambulia. Sio uamuzi sahihi kupanda mti. Wale wanaoishi karibu na eneo la msitu na wale waona fanya kilimo kwenye mipaka ya misitu wana uwezekano mkubwa wa kushambuliwa na duma.

Lakini Madhava Rao anasema: ‘’Ukivaa kinyago (kinyago kinachofanana na kichwa cha binadamu unaweza kutoroka kutoka kwenye makucha ya chui na wanyama wengine wa msituni. Kwa ujumla wanyama wa msituni hushambulia sehemu ya nyuma. Sehemu ya nyuma ya kichwa.’’

‘’Vilevile iwapo walio karibu na eneo la msitu watawasha moto usiku, chui na wanyama wengine wa msituni hawataingia msituni. Kwa ujumla makabila hufuata njia hii pia," aliongeza.

Je, duma hula watu?

Wanadamu sio kipaumbele chao katika uwindaji, isipokuwa kushambulia ikiwa wanahisi hatari. Chui wanaweza kuwa wa kwanza kukuona wanapozurura katika maeneo ya misitu. Wanyama wa porini wana uwezo wa kuhisi haraka na kunusa kuliko binadamu.

Kawaida chui ana uzito wa kilo 100 hadi 150. Na kwa kawaida duma hushambulia kwa makucha shingoni ili kunyofoa nyama ya anayewindwa. Wanajaribu kunyakua shingo kwa midomo yao. Linda shingo yako wakati akikushambulia.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live