Rapa maarufu kutoka nchini Jamaica, Diamond The Body (@diamondthebodyy) ameamua kufunga na kusema kuwa tangu apoteze usichana wake (bikra) ameshakutana kimwili na watu 2,000.
Diamond amesema alipoteza bikra yake akiwa na miaka 12, mbali na hivyo amedai kuwa haogopi wala hajali maneno ya watu na kama kuna mwanaume anataka kuwa wa 2001 ajitokeze.
Aidha, staa huyo amedai kuwa katika idadi hiyo ya watu aliolala nao wamo wanaume na wanawake, jambo ambalo limeibua mijadala mitandaoni.
“Ni Mungu pekee ndiye anayeweza kunihukumu," alisema Diamond The Body.
Utakumbuka hivi karibuni zilisambaa picha katika mitandao ya kijamii zisizo na maadili (nusu utupu) akiwa na msanii Burna Boy.