Menu ›
Burudani
Thu, 15 Sep 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Staa wa Bongo Fleva, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ amefunguka kuwa, maisha aliyoyapitia zamani yalikuwa magumu kiasi cha kulala chumba na kitanda kimoja na mama yake.
Dimpoz amefunguka hayo kupitia ukurasa wake wa Instagram akiweka kipande cha video kuelezea jinsi alivyotelekezwa na baba yake mzazi ambaye sasa hivi anaonekana kuwa ana maisha ya hali ya chini kulinganisha na Ommy.
“Sina hata kumbukumbu kwamba hili daftari labda nilinunuliwa na baba yangu. Niliishi maisha magumu nikiwa peke yangu na mama yangu. Nililala chumba kimoja na mama,” alisema Dimpoz.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live