Sakata la Harmonize na x wake Kajala linaendelea kuchukuwa sura mpya kila uchwao! Kwenye moja ya mistari aliyoishusha kwenye Insta Story yake Harmonize ni pamoja na kudai alikuwa anampa asilimia kumi ya kila anachoingiza.
Kwenye waraka huo ambao umeendelea kutrend mitandaoni, Harmonize ameeleza mambo mengi ambayo aliyafanya na Kajala licha ya kutomtaja jina lakini wafungua kodi wanaona ni dhahiri anamlenga yeye.
"Nilikuwa nakupatia asilimia kumi ya kila ninachoingiza shows, endorsment kila kitu tell them ulikuwa na pin kila kadi zangu za benki lol bahati haiji mara mbili..." aliandika Harmonize.