Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nikki wa Pili adai ushindani kwenye muziki wa Hip Hop upo kibiashara sio tungo (+video)

871 Capture 78 TZW

Mon, 1 Jan 2018 Chanzo: bongo5.com

Msanii wa Hip Hop kutoka Weusi Kampuni, Nikki wa Pili amesema muziki wa sasa wa Hip Hop ushindani wake upo kibiashara zaidi kwa kuangalia jinsi ya kuwakonga mashabiki jukwaani na namna ya msanii mwenyewe anavyoweza kujiweka kibiashara.

Nikki wa Pili amedai kuwa kinachoangaliwa kwa sasa ni kuuza bidhaa yako na bidhaa nzuri ndiyo inayouza sokoni kwa hiyo ndio muziki wa Hip Hop ya sasa ulivyo.

Akizungumzia ushindani wa Hip Hop ulivyo wa kibiashara, Nikki wa Pili amesema ni ushindani ambao Msanii mwenzako akitoa video kali na wewe unatoa video kali zaidi au akifanya show nzuri na wewe unafanya show kali zaidi yake. Msikilize Nikki wa Pili kwenye mahojiano yake na Bongo5 hapa chini

 

Chanzo: bongo5.com