height="400" Muimbaji huyo amesema mpaka sasa bado hajapata kazi ambayo anaona kuna haja ya kumtafuta msanii yeyote wa kundi hilo lilipo chini rais wa wake, Diamond Platnumz.
“Kufanya kolabo na msanii yeyote kutoka WCB inategemeana na muziki gani ambao nimeimba, naamini kila muziki una sura ambayo inaonyesha ni nani unaweza kuimba naye, ikitokea kuna muziki ambao naona kuna haja ya msanii kutoka WCB nitafanya naye na kama sina tutabaki hivi hivi WCB na Team Kiba,” Abdukiba aliimbia EFM.
Mashabiki wa muziki wanatamani siku moja kushuhudia kolabo ya msanii kutoka WCB na msanii kutoka Team Kiba.
Meneja wa Diamond, Mkubwa Fella akiahidi siku moja atahakikisha wawili hao wanafanya kolabo huku akitoa nafasi kwa upande wa Alikiba kama wataona kuna umuhimu wa kufanya hivyo.