Menu ›
Burudani
Mon, 6 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tangu mwaka jana 2022, msanii wa Bongo Movies, Niffer alikuwa akihusishwa kutoka kimapenzi na msanii mwenzake Patrick Kanumba lakini hakuna aliyeleta uthibitisho, hivyo zikabaki kuwa skendo tu.
Aliyekuja kuharibu mambo ni Mama Patrick, hivi karibuni amefanya Interview na amethibitisha kwamba wawili hawa ni wapenzi.
Baada ya kauli hiyo kutoka kwa Mama Patrick, Niffer amewaka vibaya mno, ameandika Gazeti refu sana Instagram, anadai kwamba asihusishwe na suala la kutoka kimapenzi na mtu yoyote yule, (kiufupi anamzungumzia Patrick).
Chanzo: www.tanzaniaweb.live