‘Rapa’ kutoka nchini Marekani Nick Minaj amefikiria kujumuisha nchi ya Nigeria katika ziara yake ikiwa tuu mashabiki wa nchi hiyo watajisajiri na kununua ‘tiketi’ za kutosha.
Mmoja wa shabiki nchini humo ‘ali-tweet’ kwenye moja ya post ya Nick kwa kuweka wazi kuwa Afrika imetengwa katika ziara kubwa kama hizo ambapo Nick aliweka wazi kuwa endapo mashabiki hao wako serious basi wajisajili kwa ajili ya kununua ‘tiketi’ huku akidai kuwa nchi hiyo huenda ikawa ya mwisho kwenye tour yake.
Tour hiyo aliyoipa jina la ‘Pink Friday 2 Tour' inayotaraija kufanyika mwaka 2024 ambapo kwa sasa bado ‘tiketi’ hazijatolewa lakini mashabiki wanaweza kujisajili ili tiketi zitakapotoka wawe wa kwanza kupata.