Msanii wa muziki Bongo, Q Chillah amesema licha ya kuwa na njia mbali mbali za msanii kutangaza muziki wake bado atahitaji support ya media.
Muimbaji huyo ambaye hivi karibuni ameachia ngoma mpya ‘Delailah’ ameambia FNL ya EATV kuwa ni vigumu kwa msanii kuwa juu ya media ingawa wote wanategemeana.
“Nguvu ya msanii ni kubwa ila media ina nafasi yake.” amesema Q Chillah.
“Media ni chombo muhimu sana ili msanii ajulikane ni lazima ajulikane kupitia media lakini power ya artist inawekana kwa sababu the more you push ndio unajipa fursa ya kupata nafasi nyingine ambako unatakiwa kufika,” amesisitiza.