Waswahili wanasema ‘namba’ hazidanganyi na hii imejidhihirishia siku ya juzi Alhamisi 26, 2023 katika uzinduzi wa nguo za kiume kutoka kwenye chapa ya SKIMSMENS inayomilikiwa na mfanyabiashara Kim Kardashian kwa kukusanya mamilioni ya ‘dola’ ndani ya dakika.
Vyanzo vya karibu vya mfanyabiashara huyo vinaeleza kuwa SKIMS MENS ilivunja ‘rekodi’ baada ya zaidi ya watu 20,000 kuagiza nguo ndani ya dakika tano na kufanya chapa hiyo kuingiza mamilion ya ‘dola’.
Nguo hizo za kiume zilifanyiwa ‘promo’ na mchezaji kutoka ‘klabu’ ya Al Hilal ya Saudi Arabia, Neymar akiwa na NickBosa na Shai Gilgeous-Alexander.