Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ngoma ya Rema yaweka rekodi Marekani

Rema Rema

Tue, 18 Jun 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Ngoma ya 'Calm Down' ya msanii kutoka Nigeria Rema imeweka historia ya kuwa wimbo wa kwanza kutoka Afrika kufikisha watazamaji bilioni 1 Nchini Marekani.

Mwezi wa nane mwaka 2023, ‘Calm Down remix’ aliyoifanya Rema na Selena Gomez ulikuwa wimbo wa kwanza Afrika kufikisha alama bilioni 1 katika historia ya Spotify.

Ngoma hiyo iliyomtambulisha zaidi Rema Kimataifa ilitoka mwaka 2022 na mwaka 2023 remix ya Calm Down ilipata tuzo ya Grammy katika kipengele cha wimbo bora wa Kimataifa.

Taarifa iliyotelewa na tovuti ya Daily Post News imesema kulingana na kampuni za American Music Stats, Data Chati, ‘Calm Down’ imepata zaidi ya mitiririko bilioni 1 inayohitajika nchini humo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live