Rasmi Staa wa Muziki kutoka Nchini Marekani Neyo ametangazwa kisheria kuwa Baba wa watoto wawili wa mwisho wa mpenzi wake wa zamani Sade Bagnerise baada ya majibu ya DNA kutolewa.
Staa huyo alitangazwa kama Baba wa Braiden na Brixton siku ya Ijumaa Septemba 29 baada ya uchunguzi wa DNA kutolewa na kuonesha yeye ndio baba halali wa watoto hao huku Amri ya mahakama pia ikihitaji majina ya mwisho ya watoto yabadilishwe kutoka Bagnerise ambalo ni jina la mwisho la mama yao hadi Smith ambalo ni jina la Ne-Yo.
Mwezi Mei, mwaka huu Staa huyo aliwasilisha ombi la kupimwa DNA baada ya kuhisi kuwa mtoto mdogo wa EX wake kuwa sio wake na wake ni mtoto wa kwanza ambaye ni Braiden.