Menu ›
Burudani
Mon, 10 Aug 2020
Chanzo: mtanzania.co.tz
GLORY MLAY
STAA wa Bongo Fleva kutoka visiwani Zanzibar, Nedy Music, amesema mara nyingi huwa anakwepa kumuumiza mwanamke kwa sababu gharama yake ni kubwa.
Akizungumza na MTANZANIA jana, Nedy Music, alisema jambo kubwa alilojifunza kutoka kwa wazazi wake ni kutofanya mambo ambayo yatamtoa machozi mwanamke.
“Naogopa kumuumiza mwanamke na kumfanyia chochote ambacho nahisi ataumia. Kuna muda unaweza ukawa umekosewa lakini ukaomba msamaha kwa sababu hutaki kumuona mtu huyo akiwa mnyonge au kujisikia vibaya,” alisema Nedy
Chanzo: mtanzania.co.tz