Baada ya wasanii mbalimbali kujitokeza Baraza la Sanaa Taifa, (BASATA) kufuata muongozo wa maadili katika kazi ya Sanaa msanii Nay wa Mitego naye amefika katika ofisi za uwanja wa Benjamin Mkapa na kuchukua muongozo.
Baada ya wasanii mbalimbali kujitokeza Baraza la Sanaa Taifa, (BASATA) kufuata muongozo wa maadili katika kazi ya Sanaa msanii Nay wa Mitego naye amefika katika ofisi za uwanja wa Benjamin Mkapa na kuchukua muongozo. Kupitia ukurasa wa Instagram wa BASATA wame-share picha ya msanii huyo akikabidhiwa muongozo huo na Naibu Waziri Wizara ya Sanaa, Mwana Fa jana Novemba 14, 2023 katika ofisi zilizopo Uwanja wa Benjamin Mkapa.