Wasanii wa Bongofleva, Billnass na Nandy ambao ni Wanandoa wamefanikiwa kutembelea ubalozi wa Tanzania nchini Ufaransa.
Nandy na Billnass walienda Ufaransa kwa ajili ya mapumziko ya Valentine. Billnass kupitia Insta ameandika;
Tukiwa nchini Ufaransa mimi na familia yangu tulipata wasaa wa kutembelea Ubalozi wa Tanzania Paris na tulipokelewa vizuri kwa ukarim kiasi cha kuona bado tuko nyumbani.
Lakini pia tulipata wasaa wakuona kazi nzuri zinazofanywa na Ubalozi wetu hasa katika kukitangaza kiswahili, Utamaduni na bidhaa zetu????????!!
Shukran za kipekee kwa H.E. Mr Samwel William Shelukindo, Ambassador of United Republic of Tanzania in Paris pamoja na Watendaji wote wa Ubalozi tunasema Ahsante.