Menu ›
Burudani
Mon, 19 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mrembo kutoka kwenye Bongo Fleva, Faustina Charles Mfinanga 'Nandy' amesema, Watanzania wasubiri kwani huwenda akashusha remix ya Dah ambayo ndani yake atasikika staa kutoka Marekani, Usher Raymond.
Nandy ametoa kauli hiyo mara baada ya kuulizwa na waandishi wa habari baada ya kushea mawasiliano yake na Usher waliyowasiliana kupitia mtandao wa kijamii.
"Wasubiri tu wataona kolabo ikitoka, nilishea yale mawasiliano sababu ya ule mshtuko wa msanii mkubwa kuwasiliana na mimi," alisema na Nandy.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live