Nandy The African Princess; ni malkia wa muziki wa Kizazi Kipya nchini Tanzania ambaye kwa siku tatu mfululizo alikuwa akifundwa na makungwi maarufu watatu kuelekea kwenye ndoa yake itakayofungwa Julai 16, 2022.
Nandy au Nandera anaolewa na mpenzi wake wa siku nyingi ambaye ni staa wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Billnass au Nenga.
Kwa siku tatu mfululizo, Nandy amepokea mafunzo ya ndoa kutoka kwa watangazaji na watoa elimu-rika, Miriam Migomba na Lilian Mwasha kisha akamalizia mkongwe wa muziki, Patricia Hillary.
Wote wamempa maneno kuntu kuanzia usafi wa nyumbani kwake, mwili wake na kumtunza mumuwe, Nenga.