Burudani

Habari

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Nandy, Mwijaku kimeumana, chanzo ni hiki!

Nandy Mwijaku Nandy na Mwijaku

Fri, 22 Jul 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Msanii maarufu wa Bongo Fleva, Faustina Mfinanga ‘nandy’ au ‘Mama Kijacho’ ameingia kwenye headlines na mtangazaji Burtoin Mwenda ‘Mwijaku’ baada ya audio kusambaa wakitifuana kwenye mazungumzo yao.

Taarifa za ndani kabisa zinadai kuwa wawili hao wametifuana baada ya Nandy kumuahidi Mwijaku kuwa iwapo atafanikisha moja ya dili lake na kampuni moja (jina tunalo), basi atampa Mwijaku asilimia 10 ya mapato kutokana na dili hilo.

Lakini cha kushangaza baada tu ya Nandy kusaini mkataba na kupewa mkwanja kwenye dili hilo, aliingia mitini na kumtosa mshikaji wake, Mwijaku jambo ambalo lilimkera Mwijaku na kuamua kumsaka ilia pate haki yake aliyoahidiwa.

Katika sehemu ya audio iliyovuja, inasikika sauti ya Nandy akisema; “Wewe hujaelewa, tatizo unakuwa na papara kwa kitu ambacho huelewi, hujaambiwa ten percent sijui unagawana na Msangi na wala Msangi hataki hayo mambo ya kugawana na wewe hela, na wala Msangi hataki hela, umenielewa?

Kibinadamu lazima nimpe Msangi hela kwa sababu mara ya kwanza niliongea mwenyewe kwa mdomo wangu nikasema hivi, nikipewa Tsh milioni 25, nitakupa wewe Tsh milioni 5 ugawane na Msangi.

“Sasa wewe ulitaka umpe shilingi ngapi kwenye hiyo milioni tano? Kwamba Msangi ungempa milioni moja halafu wewe ushukue milioni nne kwa sababu umetoa namba? Kwani wewe hujui kazi ya Msangi anayoifanya pale ni kazi gani?

“Angesema bosi hii kazi haitakiwi au haina maslahi, unahisi yule bosi angenipa kazi kwa sababu wewe umenipa namba? Kwani si umempeleka Zamaradi mkaenda mkaongea na mkakataliwa?,” amesema Nandy.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live