Dar es Salaam. Mwanamuziki nchini Tanzania, Faustina Mfinanga maarufu Nandy, katika tamasha lake la ‘Nandy Festival’ litakalofanyika mkoani Tanga ameamua kuchukua wasanii wa kike pekee.
Tayari wasanii mbalimbali wameshasainiwa kushiriki kwenye tamasha hilo litakalofanyika Agosti 3, 2019 akiwemo Mwasiti, Gigy Money, Amber Lulu, Isha Ramadhani, Linah na Rosa Ree huku akiahidi kuongeza wengine.
Akizungumza jana Julai 26, 2019 na Mwananchi, Nandy alisema huo ni ubunifu walioamua kuja nao na menejimenti yake kama njia ya kuonyesha wanawake wanaweza kufanya shoo wenyewe bila uwepo wa wanawake.
“Katika kulifanikisha hilo hata DJ atakuwa mwanamke ambaye ni DJ Mumy, ” alisema Nandy anayetesa na wimbo wa ‘Halleluya’ alioshirikishwa na msanii Willy Paul kutoka nchini Kenya.
Kama vile haitoshi alisema anajisikia vizuri kufanya hivyo, ukizingatia hajawahi kuona shoo ya wanawake tu huku akieleza anaamini wanawake wanaweza.
Hili ni tamasha la tatu kufanyika, likiwa limetanguliwa ni lile lililofanyika Bukoba mkoani Kagera na lile la Sumbawanga Mkoa wa Rukwa.
Pia Soma
- Mbinu za kukabiliana na udhalilishaji kazini
- Baba asimulia ulezi ulivyo na changamoto
- Zipi dalili hatari kwa watoto?
- Upungufu wa damu kwa watoto hupunguza uwezo wa kujifunza